• Webmail
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Wasiliana nasi
Kigoma District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia
    • Muundo
  • Wilaya
    • Babati
    • Mbulu
    • Hanang
    • Kiteto
    • Simanjiro
  • Idara
    • Rasilimali watu
    • Planning and Management
    • Finance and Accounts
    • Ukaguzi wa Ndani
    • Procurement and Supply
    • Economy and Production
    • Miundombinu
    • Local Government
    • Ustawi wa Jamii
    • TEHAMA
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
  • Machapisho
    • Fomu
    • Guidelines
    • Procedures
    • Ripoti
  • Investments
    • Investment One
    • Investment Two
    • Investment Three
    • Investment Four
    • Investment Five
  • Media Center
    • Habari
    • Matangazo kwa umma
    • Maktaba
    • Sports and Games
    • Hotuba
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos

TUCTA YAOMBA SERIKALI KUWATAZAMA WASTAFU WANAOLIPWABLAKI MOJA

Posted on: May 2nd, 2024

Shirikisho la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA) mkoa wa Kigoma katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi, (Mei mosi)  wameiomba serikali kuwatazama wastaafu wa zamani ambao bado wanalipwa shilingi laki moja kwa mwezi.

Akizungumza kupitia hotuba iliyoandaliwa na chama hicho, katibu wa TUCTA, Jumanne Magulu ametaja kuwa wastaafu hao wanaishi maisha magumu kutokana na hali ngumu ya uchumi na kupanda bei kwa bidhaa.

“Tunaomba serikali iwatazame kwa upya wastaafu hao, iwakumbuke na kuwaongezea kiwango cha fedha ili waweze kujikimu na kukidhi mahitaji yao, laki moja ni pesa kidogo ambayo kwa maisha ya sasa haiwezi kuwasaidia kwa muda mrefu na kuwafanya waishi maisha magumu” amesema Magulu.

Katika hotuba ya chama hicho wameziomba pia taasisi za kifedha kupunguza kiwango cha riba ya mikopo ambapo wamesema kiwango hicho hawawezi kumudu kukilipa.

Sambamba na hilo wameiomba mifuko ya hifadhi za jamii kufuatilia michango ya wanachama katika taasisi husika ili kuepusha changamoto ambazo huwa zinatokea kati ya mwajiri na mwajiriwa hasa katika kipindi cha kufuatilia mafao ambayo yalikuwa hayafikishwi katika mfuko.

Akizungumza Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambaye ni mkuu wa mkoa wa Kigoma Thobias Andengenye amewaasa wafanyakazi wote kuendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia kwa kubadili mienendo ya utendaji kazi, uwe wa juhudi na wenye maarifa ili kuinua uchumi wa nchi.

Amehimiza ushirikiano miongoni mwa wafanyakazi wote na kuachana na tabia ya ubinafsi ambayo inafanya watu kukosa haki zao huku ikichochea rushwa na utovu wa nidhamu na hivyo kuharibu utendaji kazi kwa maendeleo.

Andengenye amesema, kufuatia suala la ongezeko la mishahara ambayo ndio kauli mbiu ya maadhimisho hayo kuwa serikali inafanyia kazi mapitio ya sheria ambazo  zinakandamiza maslahi ya wafanyakazi hivyo wawe wavumilivu mpaka pale serikali utakapokamilisha mapokeo hayo.

Hata hivyo, amewaonya waajiri wanaowanyanyasa na kuwakandakiza waajiriwa, amewataka wafanye kazi kwa kufuata sheria mpya na kutekeleza haki na wajibu wa kazi, na kwamba waajiriwa wasisite kutoa taarifa kwa waajiri wa namna hiyo ili waadhibiwe sawasawa na kanuni na sheria za nchi

Latest Announcements

  • TANGAZO LA MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA

    read more
  • TANGAZO LA KAZI YA MUDA

    read more
  • TANGAZO LA MIKOPO KWA VIJANA, WANAWAKE NA WATU WENYE ULEMAVU

    read more
  • TANGAZO LA KAZI

    read more
  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA

    read more
  • View More

Habari M-pya

  • WAKULIMA WA ZAO LA MCHIKICHI WATAKIWA KUTUMIA MBEGU BORA ILI KUONGEZA UZALISHAJI NA KUKUZA KIPATO
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KIGOMA YAPIGA HATUA UTOAJI WA CHAKULA SHULENI
  • SERIKALI YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 60 KWENYE UJENZI WA MADARAJA YA MAWE KOTE NCHINI
  • DC.DKT. CHUACHUA ASISITIZA WAZAZI KUWAWEZESHA WANAFUNZI KUPATA CHAKULA SHULENI
  • DCC KIGOMA DC YAPITISHA MCHAKATO WA MGAWANYO WA KATA
  • More

Wasiliana nasi

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
THE DISTRICT EXECUTIVE DIRECTOR
Postal Address: P.O.Box 332, KIGOMA
Telephone: 028 2804865
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: 028 2804865
P.O.Box 332 KIGOMA
Postal Address: MWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA KIGOMA
Telephone: 028 280 271 9
Barua pepe: ded@kigomadc.go.tz
Mobile: +255752337486

Tovuti zinazo fanana

  • Kigoma Ujiji Mc
  • Halmashauri ya Wilaya Uvinza
  • Halmashauri ya Wilaya Buhigwe
  • Halmashauri ya Wilaya Kasulu
  • Halmashauri ya Mji wa Kasulu
  • Halmashauri ya wilaya Kibondo
  • Halmashauri ya wilaya Kakonko

Tovuti Zinazo husiana

  • OFISI YA RAIS TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI (NECTA)
  • WIZARA YA UTUMISHI NA UTAWALA BORA
  • MKOA WA KIGOMA
  • TOVUTI YA TAIFA
  • MFUMO WA MADENI YA WATUMISHI SERIKALINI
  • SALARY SLIP PORTAL

Mitandao ya Kijamii

  • Like us on Facebook
  • Follow us on Twitter
  • Find us on Youtube
  • Follow us on Instagram

Copyright ©2024GWF . All rights reserved.

  • Vigezo
  • Sera za Usiri
  • Maswali ya Mara kwa mara
  • Ramani